Pages

Monday, May 26, 2014

UTARATIBU SAHIHI WA UPAKAJI RANGI

Wafuatiliaji wa Blog yetu leo,Mwalimu anaenda kutufundisha kitu cha muhimu sana katika rangi nacho ni utaratibu sahihi wa upakaji rangi,
Somo hili haliwahusu mafundi rangi peke yao bali ni mtu yeyote anaweza kujifunza somo hili,fuatana na Mwalimu katika mtiririko huu wa somo hili.Natumaini mpaka mwisho wa somo hili utakuwa kwenye nafasi nzuri ya kujua taratibu sahihi za upakaji wa rangi
Tuanze sasa.......

        1.       Paka rangi sahihi ya kuanzia (primer)- primer itafanya kazi zifuatazo:
·         Italeta masikilizano kati ya uso na matabaka yanayo fuata.
·         Itaziba nyufa na matundu madogomadogo yaliyopo kwenye uso.
·         Italeta taswira ya uso ulivyo.


2.     Ziba mabonde yaliyojitokeza kwa uwazi kwa kijazio (putty) chenye gundi. Watengenezaji wamependekeza ya nje peke yake na ya ndani peke yake. Zipo putty za mbao na chuma pia.

        3.       Paka rangi ya kuanzia tena.
        4.       Paka rangi ya kumalizia.

Rangi ya kuanzia hutegemea  zaidi aina ya uso unaopakwa. Lakini cha kuzingatia hapa ni wapi inapakwa, yaani mazingira husika. Kama maeneo ni korofi au la. Kama eneo linachumvi, maji au kemikali isiyo koma, umakini zaidi unahitajika katika uchaguzi wa rangi ya kuanzia. Watengenezaji wanamapendekezo mbali mbali ya rangi za kuanzia kama inavyo ainishwa kwenye jedwali lifuatalo.

Aina ya uso
Aina ya primer
kiyeyushio



mbao
Wood primer
Turpentine/solvent
Metali chuma
Red oxide primer
Turpentine/solvent

Zinc phosphate/zinc chromate
Turpentine/solvent

2k epoxy hb primer, zinc rich
Epoxy thinner
Metali si chuma
2k etch primer
hakuna

Primer zote za metali chuma

Kuta za zege, tofali, mawe, saruji
Acrylic primers
maji

Undercoats za mafuta
Turpentine/solvent

Pliolite based primers
Turpentine/solvents


Nafiki mpaka kufikia hapo msomaji wetu kuna kitu utakuwa umejifunza.
Mpaka wakati mwingine tuonane tena katika mwendelezo wa somo letu.

1 comment:

Anonymous said...

Very good for this class byeee