Pages

Friday, October 11, 2013

MASOMO JUU YA RANGI YANAENDELEA

Kabla ya Chochote ni maelekezo,Mwalimu Mpoki akitoa maelekezo kabla ya kuingia kwenye vitendo


Sasa ni vitendo,Mafundi rangi za magari wakifanya kwa vitendo jinsi ya kupaka rangi za magari

Mwalimu akionyesha jinsi ya Kuchanganya Rangi

Hata wamama hawakubakia nyumba kwenye Kupata Ujuzi mpya juu ya Rangi











Sunday, October 6, 2013

SOMO KUHUSU RANGI

Tunapaka rangi kwa lengo kubwa moja, kulinda vifaa vya ujenzi vilivyo tumika kujenga majengo. Vifaa hivi vimegawanyika makundi matatatu. mbao, metali na zege.


vifaa hivi huathiriiwa na mambo ya mazingira kama joto, baridi, kemikali, vimelea na maji maji
Ziko njia nyingi za kuhifadhi vifaa hivi, njia bora na rahisi ni kuvipaka rangi.

hebu tujiulize kwanza, tunalinda dhidi ya nini? mazingira yana mambo mengi ambayo huathiri maisha ya binadamu na vitu vilivyomo. kuwenye mazingira kuna joto, baridi, maji, kemikali na hewa mbalimbali. ukivichunguza vitu hivi kwa makini utajua athari zake kwa vifaa vya ujenzi.



Mbao huliwa na vimelea, huoza na hupasuka jua linapokuwa kali. Chuma hutafunwa na kemikali kama vile tindikali, alkali na chumvi. Kuta huliwa na vimelea na chumvi na kusababisha kupungua kwa thamani yake.

Zipo namna nyingi za kufanya ili kudhibiti hali hizo kutokea. 
Wengine hutumia njia kadhaa kama hizi:
·         Mabati yaliyopakwa rangi kabla
·         Vigae na marumaru
·         Vioo
·         Karatasi
·         Mawe.


Pamoja na kuwepo kwa vitu hivi mbadala rangi ni kitu pekee na rahisi kukitumia ili kuvihifadhi vifaa hivi.

Endelea kufuatilia mwendelezo wa somo hili wiki ijayo
Na Mwl.Mpoki.