Bado tunaendelea na mfululizo wa masomo yetu kuhusu rangi,Leo tuko sehemu ya tatu katika somo letu kuhusu rangi
Fuatana na Mwalimu uweze kujua kwa undani kuhusu rangi na baadae jinsi sahihi ya upakaji wa rangi
Fuatana na Mwalimu uweze kujua kwa undani kuhusu rangi na baadae jinsi sahihi ya upakaji wa rangi
Kwangua vizuri nyuso
zilizo athiriwa kisha paka dawa ya kuwaua kabisa kabla ya kuendelea kupaka
rangi. Dawa hizi zipo aina mbalimbali km antifungal wash au biocidal wash.
Uso wenyewe pia ni uchafu. Hauna masikilizano na rangi hata
kama ni msafi kwa kuuangalia. Ni vigumu kuuondoa na kuuosha kwani ndio tunao upaka rangi. Utaratibu
sahihi wa upakaji ndio suluhisho la uchafu huu.
![]() |
| Kuta zilizoharibiwa |
KWA NINI TUPAKE RANGI
Kuna lengo kuu moja
tu la kupaka rangi, ulinzi. Hata hivyo
tunapolinda hujikuta tuna pamba pia.
ULINZI DHIDI YA NINI?
Kwenye mazingira kuna
vitu kadhaa vinavyo weza kuathiri vifaa vyetu vya ujenzi. Vitu hivi hubadilili
tabia za vifaa hivi na kuvipunguzia thamani. Vitu hivi ni kama vifuatavyo:
1.
Joto
2.
Baridi
3.
Maji
4.
Kemikali
5.
Ukungu
6.
Vimelea
7.
Hewa.
Kama hivi vinaweza kuathiri viumbe hai basi vitaharibu
kabisa vifaa vya ujenzi iwapo havita dhibitiwa.
Matabaka ya rangi yaliyo pakwa kwa ustadi yanatosha kuweka
uzio ili maadui hawa wasipenye.
Rangi haipakwi tu kwa mazoea kwa lengo la kulisafisha eneo
kama wengine wanavyodhani, bali ni taaluma yenye kanuni maalumu. Kanuni hizi
zikifuatwa vema, huleta matokeo yaliyokusudiwa. Kabla ya yote kanuni kuu ni
kuusafisha uso usiwe na uchafu wowote kama ilivyo elekezwa hapo juu. Kanuni ya
pili ni dhana ya uso ni uchafu na kutufanya tupake rangi kwa utaratibu ili
ishike kwenye uso husika.
Kwa leo tunaishia hapa,usikose juma lijalo ambapo tunataelezea jinsi sahihi ya upakaji wa rangi
.jpg)














.jpg)











